Kama ilivyotangazwa na kamati yetu ya uchaguzi leo tumeanza rasmi mchakato wa uchaguzi wetu.
Hiki ni kipindi muhimu kwa ustawi wa mpira wetu.
Ninaomba
niwahakikishie wadau wa mpira wa miguu Tanzania kuwa Sekretarieti ya
TFF ambayo kikatiba ninaisimamia mimi itaendelea na shughuli zake bila
kuathiriwa na mchakato huu, hii itakuwa ni pamoja na kuandaa timu zetu
mbalimbali za Taifa na kushughulikia majukumu yake mengine ya kila siku.
Aidha
ninaomba niwahakikishie viongozi na wadau wa mpira wa miguu Tanzania
kuwa mimi kama Rais wa TFF sina kundi katika uchaguzi huu.
Msimamo
wangu ni kuwa wagombea wote wana haki sawa na sanduku la kura ndilo
litaamua nani ataongoza mpira wetu kwa kipindi cha 2017-2021.
Wagombea wote ninawatakia kila la kheri na Mola awabariki na kuwaongoza.
Ahsanteni
Jamal Emil Malinzi
Rais wa TFF
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment