Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 21 June 2017

MAUAJI TENA KIBITI, TRAFIKI WAWILI WAHOFIWA KUUAWA MCHANA WA LEO



TAARIFA kutoka Mkoani Pwani zinaarifu kuwa Polisi wawili wa Kikosi cha Usalama wa Barabarani Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani, wanahofiwa kufa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakiwa kazini.

Majina na vyeo vya askari hao bado havijafahamika na inaelezwa kuwa wameuawa katika Kijiji cha Msafiri, Kata ya Bungu B kwenye kituo cha ukaguzi wa magari.

Inadaiwa kuwa, mbali na kuuawa kwa polisi hao lakini pia wauaji wamechoma moto gari na pikipiki za polisi hao na wamekimbia.

Kumekua na mauaji mara kwa mara ya wananchi wakiwemo viongozi na Polisi katika maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Rufiji Mkoani Pwani. 

Endelea kufuatilia Daily News-Habarileo Blog itakuletea raarifa zaidi.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment