Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 16 May 2017

MPOGOLO AANZA ZIARA YA KUIMARISHA CHAMA MKOA WA DAR ES SALAAM

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Lodrick Mpogolo, akizungumza na wanachama na Viongozi wa CCM Kata ya Manzese, wakati akiwa katika mfululizo wa ziara zake za kuimarisha Chama, ambapo leo amenza rasmi katika Mkoa wa Dar es Salaam.
****************************
Na Ripota waMafoto Blog, Dar

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema mapandikizi ya upinzani na masalia ya wasaliti hawatapenya kwenye 








uchaguzi unaoendelea ndani ya Chama kwa kuwa njama zao 








zimeshabainika. 
Kimesema kina taarifa kwamba waliotimuliwa CCM nao 
wanapanga safu za viongozi kwenye uchaguzi, lakini Chama 
kimejipanga vizuri katika kuchuja wagombea hivyo wenye nia 
hiyo hawatafanikiwa. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Rodrick Mpogolo, alisema 
hayo jana alipozungumza na wanachama na viongozi wa Chama 
katika ukumbi wa CCM kata ya Manzese wilayani Ubungo,Dar 
es Salaam. 
Alisema kuna mapandikizi kutoka upinzani wanajipanga 
kugombea uongozi CCM jambo ambalo linafahamika hivyo 
hakuna atakayepenya na hatutaruhusu 'virusi' kwa namna 
yoyote ile. 
Mpogolo pia aliwaonya viongozi wa CCM wanaondekeza ugomvi 
ndani ya Chama na kuwataka wakatafute vyama vingine 
ambavyo ni maarufu kwa kugombana hadi kutwangana ngumi.
Alisema katika mageuzi yanayofanyika sasa Chama 
hakitaruhusu viongozi wa aina hiyo kuendelea kuvuruga a
mani, kuwachafua na kuwakandamiza wanachama wenzao. 
Mpogolo alisema viongozi wenye hulka ya ugomvi, 
kukandamiza wanachama ndio chanzo cha kupunguza kura za 
CCM katika uchaguzi, hivyo Chama hakipo tayari 
kuwavumilia.
''Viongozi hawa wanajulikana, kama hawawezi kubadilika, 
waende wakajiunge na vyama vingine ambavyo ni maarufu kwa 
kupigana. CCM tunahitaji kujenga umoja na upendo baina 
yetu maana ndio silaha ya ushindi, "alisema. 
Mpogolo alisema viongozi hao wameumiza wana CCM hadi 
wengine wakaenda upinzani jambo ambalo kwenye CCM mpya na 
Tanzania, hawana fursa ya kuendelea kutesa wenzao. 
 katika hatua nyingine Mpogolo aliwataka wana CCM ambao 
wanamuwaza aliyekuwa Waziri Mkuu, na mgombea urais wa 
Ukawa Edward Lowassa, wasipoteze muda wao kwa kuwa huu ni 
wakati Rais Dk. John Magufuli. 
"Naona kuna watu bado wanawaza Ukawa, wengine bado 
wanafikiria mtu fulani. Ndugu zangu hii ni CCM mpya, 
hakuna Lowassa wala Ukawa. Nimepita mikoa 26,Watanzania 
wanasema hawataki upinzani, "alisema. 
Mpogolo alipiga marufuku uendeshaji wa vikao vya 
kushughulika na badala yake wafanye vikao vya kujenga 
Chama, na katika kipindi hiki cha uchaguzi wa CCM, 
wajielekeze kuchagua viongozi bora wasiotokana na rushwa. 
Alisema CCM inatakiwa kuwa mfano katika kudhibiti rushwa 
na kujenga nidhamu kwa viongozi na wanachama, ili iendelee  
kuwa kimbilio la wanyonge na Watanzania kwa ujumla.
Mpogolo alisema Chama kina kazi ya kukomboa majimbo ya Dar 
es Salaam yaliyokwenda upinzani, hivyo uchaguzi ndani ya 
hama unapaswa kufanyika kwa umakini mkubwa ili kupata 
safu za viongozi wa CCM watakaofanya kazi ya kumaliza 
upinzani. 
Kabla ya kuzungumza na viongozi hao Mpogolo, alikutana na
viongozi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kabla ya kukutana na 
kamati ya siasa ya Wilaya ya Kinondoni na Ubungo ambako 
alipatiwa taarifa ya Chama ikiwemo maendeleo ya uchaguzi 
katika ngazi za mashina.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Lodrick Mpogolo, akisalimiana na Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu UDSM, wakati alipowasili Kata ya Msasani Tawi la Mikoroshini leo jioni akiwa katika mfululizo wa ziara zake za kuimarisha Chama, ambapo jana amenza rasmi katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Baadhi ya wanachama wakifurahia maneno yaliyokuwa yakiongewa na Mpoglo.
Mpogolo akipunga mikono kuwaaga wanachama
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Lodrick Mpogolo, akizungumza na wanachama na Viongozi wa CCM Kata ya Msasani Tawi la Mikoroshini, wakati akiwa katika mfululizo wa ziara zake za kuimarisha Chama
Mpogolo akizungumza na wanachama.
Wanachama wa Msasani
Mpogolo akiagana na wanachama baada ya kumaliza kuhutubia.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment