Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 27 March 2017

SERIKALI YAAGIZA NEY WA MITEGO AACHIWE, WIMBO WAKE WA 'WAPO' URUHUSUWE ILA AZIDI KUUBORESHA

Na Mroki Mroki, Dodoma
SERIKALI imeagiza Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Emmanuel Elibariki ‘Ney wa Mitego’ aliyekuwa akishikiliwa na Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa mahojiano kuachiwa huru.
Agizo hilo limetolewa leo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, wakati akiongea na waandishi wa habari mjini Dodoma na kusema kuwa hata wimbo anaotuhumiwa nao kuwa umekiuka maadili uendelee kupigwa.

Msanii Ney alikuwa akishikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kumkamata juzi mkoani Morogoro na kumsafirisha hadi jijini Dar es Salaam kufuatia amri ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kile kilichodaiwa ni wimbo huo kukosa maudhui na kukiuka sharia za Basata.

Waziri Mwakyembe alifuatilia sakata hilo la kukamatwa Ney na baadae Basata kufahamisha sababu za kumkamata na kutakiwa kuhojiwa juu ya nyimbo yake ya ‘Wapo’ lakini pia Rais alimuagiza kugfuatilia suala hilo na kuona namna ya kulimaliza kwakuwa haoni kosa katika wimbo huo.

Aidha Mwakweye amesema Rais Magufuli aliomba Ney achiwe hivyo nayeye akiliagiza Jeshi la Polisi kumuachia huru msanii huyo

“Baada ya kuzungumza na Rais Dk John Magufuli ambaye yeye binafsi ameonesha wazi kuupenda wimbo huo kutokana na mindundo yake nimesha BASATA kuondoa zuio lake dhidi ya wimbo huo, na badala yake uendelee kupigwa tu kama nyimbo nyingine,”alisema Mwakembe.

Waziri Mwakyembe alisema katika mazungumzo yake na Rais Magufuli alionesha kufurahishwa na wimbo huo wa WAPO, na kumshauri Msanii huyo kama inawezekana aendelee kutaja watu wengine kama vile Wakwepa  Kodi, Wauza Unga, Wabwia Unga, Wezi pamoja na watu wengine wasio na maadili mema katika jamii.

Pia alisema alichofanya Ney wa Mitego katika wimbo wake huo ni kutumia Uhuru wa Kujieleza hivyo Rais alisema endapo Mtu anafanya kitu cha manna hiyo na hajavunja sharia hakuna haja ya kumzuia.

Akizungumza kisheria alisema Basata inamamlaka ya kufanya ilicho fanya kwakuwa ni eneo lake hata yeye Waziri hawezi kutoa agizo kwa basata ila anawaomba tu wamwachilie msanii huyo na wimbo wake kuendelea kupigwa.

Mwakyembe pia amemwomba Msanii Ney wa Mitego kesho akitane nae mjini Dodoma kwa mazungumzo na kumshauri maeneo ya kuongeza katika wimbo wake huo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment