Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 29 March 2017

CCM YAPITISHA 12 KUWANIA UBUNGE KATIKA BUNGE LA JUMUIA YA AFRIKA MASHARIKI (EALA)



 Dk.Abdallah Hasnu Makame


 Fancy Nkuhi
 Adam Kimbisa
 Zainab Kawawa
Charles Makongongo Nyerere 
********
KAMATI Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imepitisha majina 12 ya Wanachama wake walioomba kugombea Ubunge katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Jumla ya wana CCM 450 waliomba ridhaa ya Chama kupitishwa kuweza kuwania ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) ambapo Wabunge wa chama hicho walipiga kura jana kuchuja majina hayo.

Hii leo majina 12 yaliyopitisha na Kamati Kuu yamewekwa hadharani baada ya kufanyika mchujo

Waliyopitishwa na Kamati Kuu na sasa wanasubiri kupigiwa kura na Bunge Aprili 4, mwaka huu ni Zainab Kawawa, Happines Lugiko, Fancy Nkuhi, Happines Mgalula, Ngwalu Jumanne Maghembe, Adam Kimbisa, Anamringi Macha, Charles Makongoro Nyerere, Mariam Usi Yahya, Rabia Abdalh Hamid, Dk. Abdallah Hasnu Makame na Mohamed Yusuf Nuh.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment