Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 20 January 2017

MHARIRI MTENDAJI TSN AMTEMBELEA BALOZI WA AFRIKA KUSINI NCHINI

Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi akikabidhi zawadi ya shajara kwa Balozi wa Afrika Kusini nchini, Thamsaqa Mseleku alipokutana naye ofisini kwake Ubalozini Dar es Salaam kwa mazungumzo jana. Kushoto ni Naibu Mhariri Mtendaji, Tuma Abdallah na Balozi Mdogo, Patiwe Mokoena. Dk Yonazi na Naibu wake walimtembelea Balozi huyo ofisini kwake jana kwa mazungumzo ya kikazi.
Naibu Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Tuma Abdallah akisalimiana na Balozi wa Afrika Kusini nchini, Thamsanqa Mseleku wakati yeye na Mhariri Mtendaji, Dk Jim Yonazi (katikati) walipomtembelea Balozi huyo ofisini kwake jana jijini Dar es Salaam jana kwa mazungumzo. 
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi akisalimiana na Balozi mdogo wa Afrika Kusini nchini, Patiwe Mokoena wakati yeye na Naibu Mhariri, Tuma Abdallah walipokutana na Balozi wa Afrika Kusini nchini, Thamsanqa Mseleku (katikati) ofisini kwake, Dar es Salaam jana kwa mazungumzo.Picha: Fadhili Akida.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment