Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 16 January 2017

DC KAKONKO ALITAKA BARAZA LA MADIWANI KUBUNI VYANZO VIPYA VYA MAPATO AMBAVYO HAVIWAUMIZI WANANCHI

MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagaraakizungumza katika kikao Cha Baraza la Madiwani Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma.
Baadhi ya Madiwani wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kakonko.
Na FK Blog Kigoma,
MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagara ameliomba baraza  la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko  na Mkurugenzi  kubuni vyanzo ambavyo havita waumiza wananchi katika uchangiaji na kuwashirikisha Wananchi katika Shughuri za maendeleo ilikuhakikisha bajeti iliyo pangwa ya mwaka 2017-2018 inafanikiwa kwa asilimia 88% ya bajeti iliyopangwa kwa ukusanyaji mapato ipasavyo.

Pia aliwaomba Madiwani wa upinzani kuacha tabia ya kupinga rasimu ya pendekezo la bajeti iliyopendekezwa ya mwaka 2017-2018 pasipokuwa na hoja ya msingi ikiwa ni pamoja na kupinga kodi ya majengo ya kila mwananchi kuchangia kiasi cha shilingi 5000 kwa mwaka hali inayopelekea halmashauri hiyo kushindwa kuwa na vyanzo vingi vya mapato.

Rai hiyo aliitoa Jana (Leo) katika kikao cha baraza la  madiwani cha kuipitia na   kupitisha rasimu ya bajeti inayo pendekezwa na balaza hill ambapo Ndagara aliwaomba madiwani kuwashawishi Wananchi kuchangiq shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kuchangia Ujenzi wa  vyumba vya madarasa na kuchangia michango mingine iliyopendekezwa kwenye rasimu ilikufikia lengo la kukusanya mapato kwa asilimia 80%.

Aidha Ndagara aliwaomba madiwani kwa kushirikiana na Mkurugenzi kubuni vyanzo vipya vya mapato ya ndani ilikuepuka viporo vilivyo baki kwa bajeti ya mwaka uliopitq ambapo halmashauri hiyo ilishindwa kufikia lengo na kukusanya mapato kwa asilimia 28% kutokana na kukosekana kwa vyanzo vipya vya mapato katika Wilaya.

"Ushauri wangu katika baraza hili  kwenye hii bajeti mlio ipitisha nilazima kuwa na vipaumbele ilikuepuka hivi vipolo vilivyo baki niungane na Afisa mipango, tuwqshirikishe Wananchi kwa nguvu kubwa na tuache kuitegemea serikali siku zote lazima tukusanye kodi ilikuweza kuipatia halmashauri mapato kuacha kuweka vipingamizi visivyo kuwa na msingi ", alisema Kanali Ndagara.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Lusubiro Mwakabibi aliwaomba madiWani kuikataa bajeti kwa hoja ya msingi, kupinga suala la kila mwananchi kuchangia shilingi 5000 kwa mwaka ni kupinga maendeleo hakuna mwananchi anaeweza kukosa kiasi hicho cha hela kwa mwaka suala la  msingi tuongeze vyanzo vya ukusanyaji wa mapato.

Mwakabibi alisema Madiwani wanatakiwa kuwaelimisha Wananchi juu ya ulipaji modi na kuchangia  mapato ya serikali, halmashauri ya kakonko ni halmashauri ya mwisho katika ukusanyaji wa mapato nchini kutokana na vyanzo vidogo vya ukusanyaji mapato halmashauri baada ya kuliona hill imeandaa vyanzo vipya vya mapato ilikuhakikisha mapato yanaongwezeka.

Nae Mwenyekiti wa halmashauri ya Kakonko Juma Maganga alisema halmashauri imeandaa bajeti ya shilingi bilioni 29.7 iliyopitishwa na madiwani  ya mwaka wa fedha 2017 -2018 itakayo husisha makusanyo ya mapato ya ndani na fedha kutoka Serikali kuu itakayo saidia kukamilisha shuguli za maendeleo ya halmashauri hiyo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment