Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 18 May 2018

MAJALIWA AFUNGUA SEMINA ENDELEVU YA 29 YA BODI YA USAJILI WA WABUNIFU MAJENGO NA WAKADIRIAJI MAJENZI JIJINI DODMA

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Semina Endelevu  ya 29 ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu  Majengo na Wakadiriaji Majenzi kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akioneshwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa, Makame Mbarawa mashine 10 za kufyatua matofali alizokabidhiwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kabla ya kufungua semina ya Bodi hiyo kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018. Mashine hizo zitagawiwa bure kwa vikundi vinavyojishugulisha na ufyatuaji matofali. Watatu kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge na wanne kuil ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Joseph Nyamhanga.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Ofisa Mauzo wa Kampuni ya  Locks and Systems Limited ya Dar es salaam, Linda Mwamukonda kuhusu vitasa, bawaba na milango ya kielektroniki wakati alipotembelea banda la kampuni hiyo katika maonesho yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kwenye viwanja vya Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018. 
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akizungumza  kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufungua Semina Endelevu  ya 29 ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu  Majengo na Wakadiriaji Majenzi kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018.
 Baadhi ya washiriki wa   Semina Endelevu  ya 29 ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu  Majengo na Wakadiriaji Majenzi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua semina hiyo kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea ngao ya shukurani kutoka  kwa Mwenyekiti  wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, Dkt. Ludigija Boniface Bulamile baada ya kufungua semina Endelevu ya 29 ya Bodi hiyo  kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akiagana na viongozi walioshiriki katika Semina Endelevu ya 29 ya Bodi ya Usajili  wa  Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi baada ya kufungua semina hiyo kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 18, 2018. Kutoka kushoto ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi  na Mawasiliano, Profesa, Makame Mbarawa, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi, Joseph Nyamhanga na Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi Dkt. Ludigija Boniface Butamile.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment