Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 22 January 2018

Salum Njwete ‘Scorpion’ ahukumiwa jela miaka 7 na faini ya Milioni 30

Na Francisca Emmanuel
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imemuhukumu Mwalimu wa Sanaa ya kujihami, 'Martial arts' Salum Njwete maarufu kama  Scorpion, kutumikia kifungo cha miaka saba jela   na faini ya Sh milioni 30.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Ilala, Flora Haule baada ya Scorpion kupatikana na hatia katika kesi ya kujeruhi ikiwemo kumtoboa macho kinyozi, Said Mrisho.

Hata hivyo, mahakama hiyo ilimuachia huru kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

Oktoba 31,2017, Mahakama hiyo ilisema Salum Njwete  anakesi ya kujibu ambayo ni Unyanganyi wa kutumia Silaha na kujeruhi.

Scorpion alidaiwa kutenda kosa alilohukumiwa nalo Septemba 6,2016 katika eneo la Buguruni Jijini Dar es Salaam.

Upande wa mashitaka katika kesi hiyo ulikuwa na mashahidi 10 huku Mshitakiwa aliyekuwa akitetewa na Wakili Juma Nassoro alikuwa na mashahidi wawili.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment