Mahujaji kutoka sehemu mbalimbali nchini takribani 100 ambao wamekwama
katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es
Salaam kwenda hija wakiwa uwanjani hapo usiku huu pasipo kujua hatma ya
safari yao hiyo ya kwenda kutimiza ibada ya Hija, katika Mtakatifu wa
Makkah, Saud Arabia baada ya kudai kutapeliwa na waliokuwa wakiratibu
safari yao kupitia taasisi za Taiba Hajj
& Umrah Social Service Trust na Jamarat Hajj and Umrah Traveller (Picha na Katuma Masamba).
Mahujaji kutoka sehemu mbalimbali nchini takribani 100 ambao wamekwama
katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es
Salaam kwenda hija wakiwa uwanjani hapo usiku huu pasipo kujua hatma ya
safari yao hiyo ya kwenda kutimiza ibada ya Hija, katika Mtakatifu wa
Makkah, Saud Arabia baada ya kudai kutapeliwa na waliokuwa wakiratibu
safari yao kupitia taasisi za Taiba Hajj
& Umrah Social Service Trust na Jamarat Hajj and Umrah Traveller
MAHUJAJI takribani 100 wamekwama katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jiji Dar es Salaam kwenda kufanya Hijja katika mji Mtakatifu wa
Makka kutokana na taasisi zilizotakiwa kuwasafirishwa kushindwa kufanya hivyo. Anaandika Katuma Masamba.
Mahujaji hao ambao walitakiwa kuondoka leo wameshindwa
kuondoka baada ya kuwepo sintofahamu huku viongozi wa Taasisi ya Taiba Hajj
& Umrah Social Service Trust na Jamarat Hajj and Umrah Traveller hali
iliyowafanya mahujaji hao kutofahamu hatma yao.
Akizungumza na TSN Digital uwanja hapa, Mufti Mkuu wa
Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amewataka Mahujaji hao kuwa na subira wakati
wakitafuta namna ya wao kuweza kusafiri ka ajili ya kwenda kutekeleza Ibada ya
Hijja ambayo ni nguzo ya tano katika Nguzo za Kiislamu.
"Kipindi hiki mpaka kesho tunatarajia kupata majibu
yoyote kutokana juhudi za viongozi, naomba mstahamili tufanye subira tuone tutafikia wapi...mimi nitaendelea
kufuatilia kuona safari inakamilika kiasi gani kupitia viongozi, kuna wengine
hatujawapata hadi sasa lakini tunawatafuta," amesema Mufti.
Aidha, amewatoa hofu Mahujaji hao kuwa mipaka ya Mji wa
Makka kufungwa usiku wa kuamkia Jumapili, hivyo muda bado upo wa kuweza kupata
safari na kuwataka mahujaji hao kufanya dua na kumuomba Mungu ili waweze
kutekeleze ibada hiyo.
Akizungumzia hatua ya kutekelezwa uwanjani hapo, Hussein
Said Seif ambaye ametokea mkoani Mwanza amesema alilipa Sh milioni 8.5 kwa
taasisi ta Taibah ili aweze kutekeleza ibada hiyo lakini hadi usiku hakuna
jambo linaloeleweka ambapo ameshauri serikali kuchukua hatua dhidi ya taasisi
za aina hiyo.
Naye, Ummy Sekibo
mkazi wa Dar es Salaam amesema, hali imewasikitisha wananchi na waislamu
wote kwa ujumla kwani kitendo hicho si jambo jema na kwamba taasisi hiyo
inapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo ya kufutiwa usajili wake.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment