Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 7 July 2017

WHC IMEJIPANGA VILIVYO KUWAWEZESHA WATUMISHI WA KADA YA CHINI NA KATI KUMILIKI NYUMBA.

Miongoni mwa Taaisi ambazo zimeshiriki maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam mwaka huu ni Taasisi ya Ujenzi wa Nyumba za Watumishi wa Umma (WHC)  ambayo ipo katika Banda la Jakaya Kikwete. Leo hii katika kilele cha Siku kuu ya Sabasaba, Ofisa Mtendaji Mkuu wa WHC, Dk Fred Msemwa aliongoza timu ya watumishi wa taasisi hiyo kusikiliza wananchi mbalimbali waliotembelea banda hilo kwa lengo la kujua nini WHC inakifanya katika kuwapa wananchi hasa watumishi wa umma makazi bora na salama.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa WHC, Dk Fred Msemwa akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Taasisi hiyo waliokuwa wakihudumia wananchi waliotembelea Banda lao hii leo. Kulia ni  Ofisa Mauzo, Irene Kasanda na kushoto ni Ofisa Uhusiano na Mauzo, Marijane Makawia.
 

Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angelina Mabula akipata maelezo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na Watumishi Housing kutoka Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Bwana Raphael Mwabuponde alipotembelea banda lao katika maonesho ya kibiashara ya sabasaba.
 Kulia ni  Ofisa Mauzo, Irene Kasanda na kushoto ni Ofisa Uhusiano na Mauzo, Marijane Makawia wakihudumia wananchi mbalimbali waliotembelea banda hilo hii leo./Picha: Mroki Mroki

TAASISI ya Ujenzi wa Nyumba za Watumishi wa Umma (WHC) imesema imejipanga kuwawezesha watumishi wa umma hasa kada ya chini na kada ya kati kumiliki nyumba kwa gharama nafuu. Anaandika Katuma Masamba.

Ofisa Mtendaji Mkuu, Dk Fred Msemwa ameyasema hayo leo katika maonesho ya 41 ya kimataifa ya biashara Dar es Salaan (DITF) maarufu kama Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Julius Nyerere, barabara ya Kilwa.

Amesema wamepanga kuwawezesha watumishi wa umma kummiliki nyumba hizo kupitia mpango wa mpangaji mnunuzi ambao mtumishi anaweza kununua nyumba kwa mtindo wa kuanza kuwa mpangaji na hatimaye kuwa mmiliki.

"Tumekuja na mpango wa mpangaji mnunuzi, mtumishi badala ya kwenda kupanga nyumba ya kawaida na wakati huo anasubiri kujenga, anaweza kuja kwetu na fedha ambayo angetumia kupanga kwingine, ndio anatumia kupanga kwetu hadi mwisho nyumba inakuwa mali yake," amesema Dk Msemwa.

Aidha, amesema wameboresha huduma na kufanya ubunifu ili kuhakikisha Watanzania wanapata makazi bora kwa gharama nafuu.

Naye,  Ofisa Mahusiano na Masoko wa WHC, Maryjane Makawia amesema, kwa sasa wanatekeleza mradi wa makazi mkoani Dodoma ambao utawawezesha watumishibwa umma wengi kumiliki nyumba.

Amesema mradi huo utahusisha ujenzi wa nyumba 460 ambapo awamu ya kwanza zitajengwa nyumba 159.

Maryjane pia ameongeza kuwa, kipindi cha nyuma Watanzania waishio nje ya nchi walikuwa wanakosa fursa ya kumiliki nyumba nchini lakini kwa sasa taasisi hiyo imekuja na mpango wa kuwawezesha Diaspora kumiliki nyumba nchini.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment