Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 2 June 2017

WABUNGE 9 WAUNDA KAMATI KUCHUNGUZA MADINI YA TANZANITE

BUNGE limetoa waraka namba mbili kwa ajili ya kuunda kamati maalum ya wabunge tisa watakaochunguza mwenendo mzima wa madini ya Tanzanianite ili kuona namna madini hayo yanavyonufaisha watanzania.Anaandika Halima Mlacha kutoka Bungeni Dodoma.
  
Wabunge walioteuliwa kuwa katika kamati hiyo kuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Dotto Biteko, mbunge wa Rufiji Mohamed Mchengerwa (CCM), mbunge wa Msalala Ezekiel Maige (CCM) na mbunge wa Muheza Balozi Adadi Rajabu (CCM).

Wabunge wengine ni mbunge wa Viti Maalum,  Mary Mwanjelwa (CCM), mbunge wa vitimaalum Subira Mgalu (CCM), mbunge wa Ole Juma Hamad Omar (CUF), mbunge wa viti maalum Lathifa Chande (Chadema) na mbunge wa Simanjiro James Millya (Chadema).

Alitaja hadidu rejea za kamati hiyo maalum kuwa ni kupitia mkataba uliopo baina ya Shirika la Madini la taifa (Stamico) na kampuni ya Tanzanite One minning na kuangalia ushiriki wa Sky Associate ili kuona manufaa ambayo nchi inapata kutokana na madini hayo ambayo ni ghali zaidi duniani.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment