Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 2 June 2017

MALINZI:TUNGETUMIA KANUNI ZA CAF SIMBA INGEKUWA BINGWA

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jamal Malinzi amesema watafanya marekebisho ya kanuni za soka ili ziendane na zile za Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF).
Malinzi aliyasema hayo wakati akitoa shukrani kwa Rais na uongozi wa Serikali na watanzania kwa jinsi walivyoiunga mkono timu ya Taifa ya Vijana waliochini ya miaka 17 ‘Serengeti boys’ iliyoshiriki Fainali za 12 za Vijana zilizofanyika nchini Gabon kuanzia Mei 14-28.
Akizungumza kwa hisia Malinzi alisema Serengeti boys iliondolewa kwenye mashindano katika hatua ya makundi kwa kipegele cha kuangalia mchezo mliokutana nani alimfunga (head to head) mwingine akaahidi kubadili kanuni ili ziendane na kanuni za CAF.
“Kanuni ilitumika kuiondoa Serengeti boys kwenye mashindano tungekuwa tunaitumia hapa kwetu basi Simba angekuwa bingwa wa Ligi Kuu msimu wa 2016/2017,” alisema Malinzi.
Pia Malinzi alisema watashusha mashindano ya U-20 kuwa ya wachezaji wa U-17 ili kusaidia kupatikana kwa timu za vijana imara wanaotokea kwenye klabu kuliko ilivyo sasa TFF ndio inakuwa na jukumu la kuandaa timu za vijana.
Serengeti boys katika mashindano ya AFCON U-17 ilikuwa kundi B pamoja na timu za Mali, Angola na Niger lakini ikaondolewa na Niger.
Katika mchezo wa awali Serengeti boys ilitoka suluhu na Mali, ikaifunga Angola mabao 2-1 na kufungwa na Niger bao 1-0.
Endapo TFF ilikuwa inatumia kanuni hiyo basi Simba ingekuwa bingwa kwani baada ya ligi kumalizika Simba na Yanga zilikuwa sawa kwa pointi 68 lakini ingefaidika kwani mchezo wa awali ilitoka sare ya 1-1 na raundi ya pili Simba ikashinda mabao 2-0.
Malinzi alisema anaamini kamati ya utendaji itakubali kupitisha kipengele hicho ili kuanzia msimu ujao zitumike kwenye ligi zote za TFF.
Aidha Malinzi alisema Serengeti boys itakuwa ndio timu ya U-20 ‘Ngorongoro Heroes’ ambayo zitafanyika 2019 hivyo benchi la Ufundi litaanza kambi za maandalizi kwa kucheza michezo za majaribio za nje ya nchi na ndani.
Pia Malinzi aliipongeza Zambia kwa kufuzu robo fainali ya mashindano ya Vijana ya dunia ya U-20 yanayofanyika Korea Kusini.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment