Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 30 June 2017

RAIS WA TFF JAMALI MALINZI NA RAIS WA SIMBA NA WENZAO KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUTAKATISHA FEDHA

atuhumiwa wa makosa mbalimbali yakiwapo ya kutakatisha fedha. Kutoka kushoto, Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine, Rais wa TFF, Jamal Malinzi, Mhasibu wa TFF, Nsiande Mwanga, Makamu wa Rais wa Klabu ya Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' na Rais wa Simba, Evance Aveva wakiwa katika Mahakam ya Hakimu Mkazi Kisutu kusomewa mashitaka yao Dar es Salaam jana.
Watuhumiwa wa makosa mbalimbali yakiwapo ya kutakatisha fedha. Kutoka kushoto, Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine, Rais wa TFF, Jamal Malinzi, Mhasibu wa TFF, Nsiande Mwanga, Makamu wa Rais wa Klabu ya Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' na Rais wa Simba, Evance Aveva wakiwa katika Mahakam ya Hakimu Mkazi Kisutu kusomewa mashitaka yao Dar es Salaam jana.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi pamoja na wenzake wamesomewa mashitaka 28 huku yakiwemo ya kughushi na utakatishaji fedha zaidi ya dola za Marekani 300,000.

Wengine katika kesi hiyo ni Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Nsiande Mwanga ambao wamesomewa mashitaka yao leo (Alhamisi) mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri wa Mahakama ya Hakimu Mkazi. Kisutu.

Kati ya Mashitaka hayo Malinzi pekee anakabiliwa na mashitaka 22 ya kughushi risiti mbalimbali zinazoonesha kuwa aliikopesha TFF fedha kwa nyakati tofauti, mashitaka mengine yanawahusu Selestine na Nsinde huku shitaka moja likiwahusu wote.

Akisoma hati ya mashitaka Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga kwa kusaidiana na Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Leornad Swai amedai kwa nyakati tofauti washtakiwa hao walitenda makosa hayo ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Hata hivyo, upande wa jamhuri uliomba kesi hiyo ihairishwe kwa madai upelelezi haujakamila, ambapo Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 03, mwaka huu.

Awali Mahakamani hapo Rais wa Simba Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange walipandishwa kizimbani wakikabiliwa na mashitaka matano ikiwemo ya utakatishaji fedha ambayo hayana dhamana.

Washitakiwa wote kwa pamoja wanadaiwa kutakatisha fedha ambayo ni dola za Marekani 300,000  walizozipata kwa kughushi nyaraka kuonesha kwamba Club ya Simba imelipa deni la fedha hiyo kwa Aveva.

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alisema mashitaka hayana  dhamana hivyo aliahirisha hadi Julai 13 mwaka huu kujua hatua ya upelelezi umefikia wapi.

Baada ya kesi hiyo kuahirishwa gari ya polisi iliwasili saa 10:26 na kuwachukua watuhumiwa hao pamoja na Rais wa Simba, Evance Aveva na Makamu wa Rais, Geofrey Nyange "Kaburu" ambao na wao wanakabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha dola za Marekani 300,000.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment