Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 13 June 2017

POLISI WATATOA TAHADHARI DHIDI YA MATAPELI

JESHI la Polisi Tanzania limetoa tahadhari kwa wananchi juu ya utapeli unaofanywa na kundi la watu wanaolaghai watu na kujipatia fedha kwa minajili ya kuwasaidia kujiunga na jeshi hilo. Anaandika Mroki Mroki.

Taarifa iliyo tolewa na Jeshi la Polisi kupitia kwa Msemaji wa wake, Naibu Kamishna (ACP), Advera Bulimba (pichani) ilisema kikundi kidogo cha matapeli wanazunguka katika maeneo mbalimbali hususani vijijini na kuwalaghai vijana kwamba wao ni watumishi ama waajiriwa wa Jeshi la Polisi na kujipatia fedha.

Alisema watu hao wamekuwa wakitapeli fedha hizo kutoka kwa wananchi hasa vijana kwa udanganyifu kwamba watawapatia ajira ndani ya Jeshi la Polisi jambo ambalo siyo la kweli. 

“Jeshi la Polisi nchini, linatoa tahadhari kwa  wananchi kwamba ndani ya Jeshi la Polisi hakuna ajira zilizotangazwa, na hivyo tunawataka wananchi wote kuwa makini na mtandao huo wa matapeli,”ilisema taarifa hiyo ya ACP Bulimba.

Taarifa hiyo ilisema kuwa mfumo wa ajira ndani ya Jeshi la Polisi ni wa wazi na una utaratibu maalum ambao hutangazwa kwa wananchi kwa mujibu wa taratibu za Jeshi la Polisi.

Kufuatia hali hiyo,  Jeshi la Polisi linatoa onyo kali kwa wote wenye tabia hiyo ya utapeli kuacha mara moja na endapo mtu yeyote atabainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha Polisi linatoa rai kwa wananchi wote wenye taarifa za matapeli hao kuzifikisha haraka katika kituo chochote cha Polisi kilicho karibu ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment