Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 12 June 2017

KAMATI YA MAKINIKIA YAPENDEKEZA ACACIA NA WALIOHUSIKA KATIKA MIKATABA KUCHUKULIWA HATUA

 Mwenyekiti wa Kamati ya Pili ya kuchunguza mchanga wa madini unaosafirishwa kwenda nje ya nchi (Makinikia) Prof. Nehemia Osoro akiwasilisha ripoti yake kwa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam leo. 
******************
KAMATI ya Pili ya uchunguzi wa mchanga wenye madini imependekeza serikali kupitia Msajili wa Makampuni kuichukulia hatua kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia Mine PL Cambayo imekuwa ikiendesha shughuli zake kinyume cha sheria. Anaandika Katuka Masamba-dailynewstzonline.blog.


Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Nehemia Osoro amesema, wamebaini kuwa kampuni hiyo haijasajiliwa katika taasisi yoyote nchini.


Aidha, kamati hiyo imependekeza serikali kuzuia usafirishaji wa makinikia, hadi hapo wadaiwa watakapolipa madeni yao yote na pia kuwachukulia hatua waliokuwa Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali, Manaibu na watumishi wote waliohusika katika upotevu wa mapato.


Kamati hiyo pia imependekeza, serikali ianzishe utaratibu utakaowezesha ujenzi wa kiwanda cha uchenjuaji ili kuondoa upotevu wa mapato na kutengeza ajira kwa Watanzania.


“Serikali ianzishe utaratibu wa kulinda maeneo ya migodi na viwanja vya ndege vilivyoko migodini ili kudhibiti vitendo vya hujuma zinazoweza kufanywa na baadhi ya makampuni za madini,” amesema Profesa Osoro wakati akisoma mapendekezo ya kamati hiyo.


Mapendekezo mengine yaliyowasilishwa na kamati hiyo ni, Sheria iweke kiwango maalumu ya kiwango cha hisa ambacho kitamilikiwa na serikali katika makampuni zote za madini, serikali ichunguze mwenendo wa watumishi wa Mabaraza ya Kodi kwa kuchukua muda mrefu kutoa maamuzi ya mashauri ya kodi.


Sheria itamke bayana kuwa madini ni maliasi asili ya Watanzania na iwekwe chini ya uangalizi wa Rais kwa manufaa ya Watanzania. Sheria ielekeze makampuni ya madini ziweke fedha zinazotokana na mauzo yao katika mabenki ya nchini ili kukuza uchumi wa nchi na kuondoa mianya ya ukwepoaji kodi


Profesa Osoro aliongeza kuwa, mikataba ya madini isiwe ya siri na ni lazima iridhiwe na bunge na pia serikali itoe elimu kwa watumishi wake kuhusu sekta ya madini.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment