Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 8 June 2017

DK MPANGO AWAONYA WATUMISHI TRA

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango akisoma Bungeni Mjini Dodoma leo Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018.
Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA.
**********
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amewaonya watumishi wa Mamlaka ya Mapato tanzania (TRA)  kutotumia vitisho na unyanyasaji kwa walipa kodi, kwa kuwa atakayefanya hivyo atachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma. Anandika Katuma Masamba-dailynewstzonline.blog

"Wale watumishi wa TRA ambao naamini ni wachache tu, wanaojihusisha na vitendo hivyo, wakome kabosa kufanya hivyo," amesema Dk Mpango na kushangiliwa na wabunge.

Akiwasilisha bajeti, Dk Mpango amesema matumizi ya vitisho, unyanyasaji kwa walipakodi, kuwadai rushwa au kuwazidhishia makadirio ya kodi ili kuwakomoa ni mambo ya hovyo na hayakubaliki hata kidogo.

Aidha, Dk Mpango ametoa rai kwa wafanyabiashara na wananchi wazalendo kutoa taarifa za ukweli kuhusu mwenendo mbaya wa mtumishi yeyote ili zifanyiwe kazi, pia wafanye hivyo katika kutoa taarifa za wafanyabiashara wanaokwepa kodi ili washughulikiwe ipasavyo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment