Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 2 June 2017

AASISI YA NATHAN MPANGALA FOUNDATION (NMF) KUWAJENGEAUWEZO WACHORA VIBONZO NCHINI

TAASISI ya Nathan Mpangala NMF itaendesha warsha ya siku tatu itakayofanyika katika ukumbi wa Nafasi Art Space, Dar es Salaam inakusudia kuwajengea uwezo wachora vibonzo vijana ambao tayari wanafanya kazi kwenye vyombo vya habari na wale ambao bado hawajapata nafasi hiyo. 

Kutokana na mabadiliko ya teknolojia duniani, NMF inaamini kuwa kuna umuhimu wa wachora vibonzo wakapata mafunzo ya mara kwa mara ili kuendana na mabadiliko hayo.

Mwenyekiti wa NMF, Nathan Mpangala amesema kuwa warsha hiyo itafanyika Juni 7-9 mwaka huu na itafuatiwa na onesho la wazi la vibonzo vilivyochorwa katika warsha hiyo siku ya Jumamosi, tarehe 10/6/2017 kuanzia saa 10.00 alasiri mpaka 12 jioni katika katika ukumbi huo huo ambapo wakaazi mbalimbali wanakaribishwa.  Hakutakuwa na kiingilio.

Mpangala alisema, 
NMF inayoamini kuwa kipaji kinakuwa na maana pale tu kinapoibuliwa, endelezwa, nufaisha msanii na Taifa, inatoa shukrani kwa Ubalozi wa Uswis nchini Tanzania, Nafasi Art Space na RUKA Kipro kwa kuwezesha warsha hii kufanyika.

NMF inatoa wito kwa wadau mbalimbali kuiunga mkono hasa katika eneo la kuwajengea uwezo vijana wenye ndoto ya kuja kuwa wasanii hodari nchini.
 
Nathan Mpangala Foundation (NMF), No.5286, yenye makao yake jijini Dar es Salaam, ni asasi isiyokuwa ya kiserikali iliyosajiliwa mwishoni mwa mwaka jana kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ikiwa na malengo kadhaa ikiwemo mafunzo ya sanaa.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment