Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 5 March 2017

MAGUFULI AAGIZA MAZUNGUMZO NA DANGOTE YAISHE



Na Basil Msongo
RAIS John Magufuli ameagiza kwamba, ikifika Jumatano wiki ijayo, mazungumzo  kati ya Wizara ya Nishati na Madini na bilionea Aliko Dangote yawe yamekwisha ili gesi ipatikane kwenye kiwanda cha saruji cha mfanyabiashara huyo.

Ameagiza kwamba, Wizara hiyo ijadiliane na Dangote mwenyewe badala ya kupitia kwa watu aliowaita kuwa ni matapeli.

Ametoa maagizo hayo leo kabla ya kuzindua magari 580 ya Dangote yatakayotumika kusambaza saruji kutoka kiwandani hapo.

Amewatuhumu baadhi ya wawakilishi wa mfanyabiashara huyo kuwa wanachelewesha uwekezaji na huenda wanashirikiana na viwanda vingine vya saruji kuihujumu Serikali.

“Inawezekana watu wako wanaokuwakilisha wana matatizo, hii ni meseji kwa mheshimiwa Dangote mwenyewe, ni lazima awe mwangalifu kwa watu wake”amesema Rais Magufuli.

Amesema, mfanyabiashara huyo ni mwekezaji muhimu sana Tanzania kwa kuwa amewezesha maelfu ya Watanzania kupata ajira na pia Serikali inapata mapato kupitia kodi.

Amemshukuru Dangote kwa kuwekeza Tanzania na pia amemshukuru Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kwa kusimamia mchakato uliowezesha kujengwa kwa kiwanda kikubwa cha saruji mkoani Mtwara.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment