Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akifungua wa
Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika
Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es
salaam leo.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiongea machache wakati wa
kuanza kwa hafla ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala
za Mitaa Tanzania (ALAT) katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo.
Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Bw. Gulma Hafeez
Muccadam akisoma risala yao mbele ya Rais Dkt magufuli wakati wa kuanza
kwa hafla ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 33 wa katika Ukumbi wa
Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam
leo.
Naibu
Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Mhe. Suleiman Jaffo mbele ya Rais Dkt magufuli wakati wa kuanza kwa
hafla ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 33 wa katika Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo.
Waziri
Mkuu Mhe Kassim majaliwa akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kufungua wa Mkutano Mkuu wa 33 wa
Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo.BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na meza kuu
wakipata picha ya kumbukumbu na wadau wa maendeleo na wafadhili wakuu wa
Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) baada
ya kuufungua katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere jijini Dar es salaam leo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipeana
mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker baada
ya kufungua Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania
(ALAT) katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere
jijini Dar es salaam leo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiagana na
Makamu Mwenyekiti wa ALAT Bw. Stephen Mhapa baada ya kufungua Mkutano
Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika Ukumbi
wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam
leo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiagana na
Mstahiki Meya wa Dar es salaam Mhe. Isaya Mwita Baada ya kufungua
Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika
Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es
salaam leo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akifurahia
ngoma ya Kigogo wakati akiwasili kufungua Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya
ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitembelea
banda la benki ya NMB na mabanda mengine kabla ya kufungua wa Mkutano
Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika Ukumbi
wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam
leo.
PICHA NA IKULU.
*******************
RAIS Dkt. John Magufuli amewataka viongozi
wa mamlaka za Serikali za Mitaa kuunga mkono juhudi mbalimbali zinafanywa
kutetea rasilimali za taifa, kujenga uchumi na kurekebisha dosari
zinazosababisha kero kwa wananchi ili kujenga Tanzania mpya.
Rais
Magufuli amesema hayo leo wakati akifungua mkutano mkuu wa 33 wa Jumuiya ya
Tawala za Mitaa (ALAT) unaofanyika
katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam
na kujumuisha viongozi na watendaji wakuu wa Majiji, Manispaa, Miji na
halmashauri za Wilaya.
Rais
Magufuli ametaja juhudi zilizofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano tangu
ilipoingia madarakani miezi 23 iliyopita kuwa ni pamoja na kudhibiti matumizi
yasiyo ya lazima na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali kutoka Shilingi
Bilioni 850 hadi kufikia Shilingi Trilioni 1.3, kuongeza bajeti ya maendeleo
kutoka asilimia 26 hadi kufikia asilimia 40, kutoa elimu ya msingi na sekondari
bila malipo kwa kutoka ruzuku ya Shilingi Bilioni 23.868 kila mwezi, kuongeza
bajeti katika huduma za afya na kutekeleza miradi ya maji katika miji na vijiji
mbalimbali nchini.
Juhudi
nyingine ni kuimarisha miundombinu ya usafiri kwa kuanza ujenzi wa reli ya kati
kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge)
kati ya Dar es Salaam na Morogoro na baadaye Morogoro – Dodoma kwa Shilingi
Trilioni 7, kununua ndege 6 kwa ajili ya shirika la ndege la taifa, upanuzi wa
bandari za Dar es Salaam, Mtwara na Tanga, Ununuzi wa meli mbili za ziwa Nyasa,
ujenzi wa viwanja vya ndege, barabara za juu Jijini Dar es Salaam na barabara
ya njia 6 ya Dar es Salaam – Chalinze pamoja na kuendeleza mradi wa mabasi
yaendayo haraka Jijini Dar es Salaam (BRT).
Rais
Magufuli ameongeza kuwa Serikali inaendelea na juhudi za kuongeza uzalishaji wa
umeme kutoka megawatts 1,460 zinazolishwa hivi sasa hadi kufikia megawatts
5,000 ifikapo mwaka 2020 kwa kujenga miradi ya uzalishaji umeme kwa kutumia
gesi na kujenga mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stieglers’ Gorge), kuongeza vijiji 7,873
vitakavyopata umeme na hivyo kufikia vijiji zaidi ya 12,259 ifikapo mwaka 2021,
kusimamia biashara ya madini kwa manufaa ya Watanzania, kusimamia ipasavyo
usambazaji wa pembejeo na kujenga mazingira bora ya uwekezaji.
Rais
Magufuli amewahakikishia viongozi hao kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga
kufanya juhudi kubwa zaidi zenye manufaa kwa nchi na hivyo ametoa wito kwa
viongozi hao kutoa ufafanuzi wa dhamira hiyo kwa wananchi na kushirikiana
kutekeleza mipango na miradi kwa kutanguliza maslahi ya taifa.
“Nataka
niwaambie ndugu zangu adui yetu sio vyama vya siasa, adui yetu ni wanaotuibia
rasilimali zetu, hivyo twende pamoja, tushirikiane kuijenga nchi yetu”
amesisitiza Rais Magufuli na kuwataka viongozi hao kuondoa tofauti na migogoro
iliyopo kwenye mamlaka zao.
Aidha,
Rais Magufuli amewapongeza viongozi hao kwa kazi kubwa wanayoifanya kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali na
mipango ya Serikali na amewahakikishia kuwa changamoto zinazowakabiri
zitafanyiwa kazi ili kuongeza ufanisi wa mamlaka hizo.
Mkutano
huo umehudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim
Majaliwa Majaliwa pamoja wadau mbalimbali wa maendeleo wa halmashauri kutoka
taasisi na mataifa mbalimbali.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment