Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 10 August 2017

MANISPAA YA LINDI YAOMBA MAGHALA

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga akizungumza na ugeni kutoka Benki ya Kilimo walipomtembelea Ofisi kwake mjini Lindi kuangalia miradi inayoendeshwa kibiashara mkoani humo.



Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga (kulia) akizungumza na ugeni kutoka Benki ya Kilimo walipomtembelea Ofisi kwake mjini Lindi kuangalia miradi inayoendeshwa kibiashara mkoani humo.



Maafisa kutoka Benki ya Kilimo wakifatilia kwa makini mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga (hayupo pichani). Kulia ni Afisa Mikopo Mwandamizi, Mubezi Buberwa na Afisa Usimamizi wa Mikopo, Elizabeth Kitaluta (kushoto).



Meneja wa Mikopo wa TADB, Samuel Mshote akiongea na Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga (hayupo pichani) kuhusu fursa za mikopo inayotolewa na TADB.
                                                                        ***************
Na mwandishi wetu, Lindi
Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga ameiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuwasaidia katika kujenga na kuendeleza maghala ili kuwaweza wakulima wa manispaa hiyo kuhifadhi mazao yao.

Ndemanga amesema kuwa maghala ya kuhifadhi mazao yamekuwa ni eneo lenye changamoto kubwa hali inayorudisha nyuma tija kwa wakulima wa manispaa hiyo.

Akizungumza na ugeni kutoka TADB, uliongozwa na Meneja wa Mikopo wa Benki hiyo, Samuel Mshote, Mkuu huyo wa Wilaya aliongeza kuwa kutokuwa na maghala ya kutosha katika  manispaa kumekuwa kikwazo kikuu kwa wakulima kufikia malengo yao kwa kuwa imekuwa ikiongoza gharama na upotevu mkubwa wa mazao yao.

“Changamoto ya uhaba wa maghala imesababisha manispaa kutokupata mapato stahiki kwa kuwa uhifadhi wa mazao umekuwa ukifanyika katika maghala ya watu binafsi ambayo hayakidhi mahitaji halisi ya manispaa,” alisema Ndemanga.

Aliongeza kuwa ujio wa Benki ya Kilimo utasaidia kwa kiasi kikubwa katika kutatua changamoto hiyo.

Naye, Meneja wa Mikopo wa Benki hiyo, Samuel Mshote alisema kwa kutambua changamoto zinazowakabili wakulima Benki ya Kilimo imeandaa mikopo maalumu kwa ajili ya kuendeleza miundombinu ikiwemo ujenzi wa maghala ya kuhifadhia mazao.

“Mikopo hii ni kwa ajili ya kujengea miundombinu ya aina mbalimbali kwenye mlolongo wa thamani, kwa mfano: skimu/ mifumo ya umwagiliaji, maghala ya kisasa ya kuhifadhia mazao, pamoja na mahitaji mengine ya miundombinu za kilimo,”alisema Mshote.

Kwa mujibu wa Mshote, mikopo ya aina hii itarejeshwa kwa awamu katika kipindi cha miaka 5 hadi 15.

Akifafanua zaidi Mshote alisema kuwa ukokotoaji wa marejesho huendana na uwezo wa kuilipa kwa kuzingatia mpango kazi, na hivyo kipindi kilichoridhiwa kwenye mkataba.

“Tunatambua kuwa miundombinu ya aina hii, mara nyingi thamani yake huongezeka kadiri muda unavyopita, miundombinu hiyo huhitaji uangalizi mzuri (maintenance),” alisema.   


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment