Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 14 July 2017

WAZIRI MBARAWA KUUNDA TUME KUPITIA MIKATABA YA WAFANYABIASHARA AIRPORT DAR

Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA),  Joseph Nyahende (wa pili kushoto) akitoa ufafanuzi wa namna abiria wenye viza  wanavyohudumiwa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,  Prof. Makame Mbarawa (mwenye miwani kifuani). Pembeni ya Waziri ni Katibu Mkuu sekta ya Uchukuzi, Dr. Leonard Chamuriho na nyuma mwenye suti nyeusi ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania,  Salim Msangi.

Katibu Mkuu wa chama cha madereva wa taxi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Simon Mwampashi (kulia), akitoa maoni mbalimbali kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,  Prof. Makame Mbarawa leo alipofanya ziara JNIA.


Mkuu wa Kitengo cha Idara ya Uhamiaji Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Flugence Andrew (kulia) akitoa maelezo ya utaratibu unaotumika kulipia viza kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa,  leo alipofanya ziara kwenye jengo la abiria la kiwanja hicho.
Afisa wa Benki ya NMB, Leah Rutayungurwa  (aliyendani ya dirisha) akimmsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof Makame Mbarawa aliyetaka kujua muda anaohudumiwa abiria mmoja wakati akilipia viza kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA).




Afisa Forodha Msaidizi, Hezron Giso (kulia), akielezea shughuli anazozifanya ndani ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA), kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,  Prof. Makame Mbarawa (mwenye miwani kifuani), wakati wa ziara ya Waziri iliyofanyika leo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA), mwenye kizibao akielezea jambo katika meza ya ukaguzi wa tiketi za abiria wanaosafiri. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA),  Salim Msangi.
***************

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema ataunda timu ya wataalmu kwa ajili ya kupitia mikataba ya wafanyabiashara katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa julius Nyerere (JNIA).

Ametoa kauli hiyo baada ya kukagua huduma mbalimbali katika uwanja huo wa ndege ambapo amesema, mikataba minne itaanza kupitiwa kwa kuwa inaonekana kuwa na kasoro.

"Nimeuliza kidogo lakini inaonekana analipa kila baada ya mwezi, lakini mimi ninapokodi nyumba nalipa kila baada ya mwaka, tuna changamoto kubwa ya mikataba hapa uwanja wa ndege," amesema Profesa Mbarawa.

"Kuna mikataba minne tayari nimeshaona ambayo tutayarisha timu ya wataalamu watakaopitia upya, sio tu hii hata mingine ni lazima tuweke utaratibu mzuri ambao serikali inapata fedha inayostahili na fedha hizo tukizipata tutaboresha uwanja wa ndege wa hapa," amesema.

Katika hatua nyingine, amesema pia uongozi wa uwanja huo wa ndege ni mzuri lakini hauendi na inayotakiwa, kwani uongozi unaotakiwa ni wa watu wenye uzalendo wa kukusanya kodi na pia kupeleka mbele uwanja huo.

Profesa Mbarawa amesema, uongozi wa uwanja huo pia uhakikishe unaondoa malalamiko yaliyopo ya abiria wanaoingia nchini kukaa muda mrefu katika kupata huduma.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment