Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 15 June 2017

WANANCHI 7 KATI YA 10 WANAUKUBALI UTENDAJI WA RAIS MAGUFULI



ASILIMIA 71 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais John Magufuli tangu alipoingia madarakani.

Rais anakubalika zaidi miongoni mwa makundi ya wazee na wenye kiwango kidogo cha elimu

Kiwango hiki kimeshuka kutoka asilimia 96 mwezi Juni 2016.  Viwango vya kukubalika kwa Rais vinatofautiana katika makundi mbalimbali ambapo asilimia 68 wenye umri chini ya miaka 30 wanamkubali Rais Magufuli ikilinganishwa na asilimia 82 wenye umri zaidi ya miaka 50.

Aidha asilimia 75 ya wananchi wenye elimu ya msingi au chini yake wanamkubali Rais Magufuli ikilinganishwa na asilimia 63 ya wale wenye elimu ya sekondari au zaidi na asilimia 75 ya wananchi masikini wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 66 ya wananchi matajiri.

Wakati viwango hivyo kukubalika kwa Rais vikionesha kushuka ukilinganisha na utafiti wa mwezi Juni mwaka jana, viwango vya kukubalika kwa viongozi wengine navyo pia vimeshuka katika kipindi hicho hicho.

Utafiti unaonesha kuwa Wabunge kukubalika kwao kiutendaji  kumeshuka kutoka asilimia 79 ya mwezi Juni 2016  hadi asilimia 58 ya Aprili 2017 huku Madiwani kukubalika kwa utendaji wao ukishuka kutoka asilimia 74 Juni 2016 hadi asilimia 59 ya Aprili 2017.
Kundi lingine la viongozi wa wananchi ni la Wenyeviti wa vijiji/mitaa na vitongoji ambalo  Kukubalika kwao kiutendaji kumeshuka kutoka asilimia 78 Juni 2016 hadi asilimia 66 ya Aprili 2017.
Matokeo haya yametolewa na Twaweza katika utafiti wake uitwao Matarajio na matokeo; Vipaumbele, utendaji na siasa nchini Tanzania.

Utafiti huo unatokana na takwimu kutoka Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za mikononi.
Matokeo hayo yanatokana na takwimu zilizokusanywa mwezi Aprili mwaka 2017 kutoka kwa wahojiwa 1,805 kutoka maeneo mbalimbali Tanzania Bara


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment