Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 8 June 2017

HAKUNA GHARAMA KWENYE BIDHAA ZA MTAJI



SERIKALI imeazimia kusamehe Ongezeko la Thamani kwenye bidhaa za mtaji (capital goods) ili kupunguza gharama za ununuzi na uagizaji mashine na mitambo ya kuzalishia na hivyo kuvutia uwekezaji katika sekta ya viwanda. Anandika Katuma Masamba-dailynewstzonline.blog



Hatua hiyo , itahusisha viwanda vya mafuta ya kula, nguo, ngozi, dawa cza binadamu na mifugo. Lengo la kufanya hivyo ni kuvutia wawekezaji katika sekta za viwanda, kilimo cha mazao na mifugo pia kukuza ajira na kukuza uchumi wa nchi.

"Hatua hii itawezesha viwanda vidogo na vya kati kupata unafuu wa gharama za kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani kwa mashine na mitambo watakayonunua kwa ajili ya kusindika na kutengeneza bidhaa mbalimbali," amesema Waziri wa Fedha na Mipango, DK Philip Mpango.

Amesema mitambo na mashine zote zitakazosamehewa kodi ya Ongezeko la Thamani zitaanishwa kwa kutumia HS Codes.

Aidha,  amesema serikali imeondoa kodi ya Ongezeko la Thamani kwa kiwango  katika huduma zinazotolewa kwenye usafirishaji wa bidhaa na mizigo nje ya nchi (ancillary transport services).

Kwa mujibu wa Dk Mpango lengo la hatua hiyo ni kupunguza gharama za usafirishaji katika bandari za tanzania kwa kuifanya tanzania kuwa njia bora zaidi ya kupitisha bidhaa zinazotoka nje ya nchi kwenda nchi nyingine hususan zisizo na bandari (landlocked countries).

"Hatua hii itahamasisha wasafirishaji kutoka nchi jirani kupitisha mizigo yao kwa wingi kwenye bandari zetu na hivyo kukuza uchumi wa nchi kutokana na kuongezeka kwa mapato ya bandari," amesema Dk Mpango.

Hatua hizi zote za Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa ujumla wake zinatarajiwa kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 48,034.1.

Baada ya waziri mwenye dhamana kuwasilisha bajeti hiyo, wabunge wanatarajiw akuanza mjadala Juni 12 mwaka huu kuhus mapendekezo au maboresho waliyonayo katika bajeti hiyo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment