Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 16 June 2017

CCM YARIDHISHWA NA UAMUZI WA RAIS KUZUIA

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole 
**********
Na Katuma Masamba
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimeridhishwa na uamuzi wa Rais John Magufuli wa kuzia mchanga wa madini (Makinikia) kwenda nje ya nchi ikiwa ni hatua ya kulinda rasilimali za Watanzania.

Aidha, Chama hicho kimezipongeza kamati mbili zilizokuwa zikiongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma na Profesa Nehemiah Osoro zilizoundwa kwa ajili ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu uliokuwa ukisafirishwa kwenda nje ya nchi kwa uzalendo wa kweli ambao licha ya kuwepo kwa vitisho na hongo lakini zilisimama kwa ajili ya kulinda maslahi ya Watanzania.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole wakati akizungumza na vyombo vya habari leo (Alhamisi) katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya chama hicho zilizopo Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Amesema kilichofanywa na Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM ni kuanza kuweka mifumo ya kusimamia na kukomesha utoroshwaji wa mali ya Watanzania, hatua ambayo ni sehemu ndogo ya mambo mengi ambayo yameshatekelezwa yaliyomo katika ilani ya chama hicho.

“CCM imefurahishwa na uamuzi wa Rais haukuwa uamuzi mrahisi haukuwa uamuzi mwepesi na mi nadiriki kusema kulikuwa n amashinikizo makubwa sana, lakini tumefurahishwa na msimamo dhabiti na madhubutu wa Rais na timu yake,” amesema Polepole.

Aidha, ameelezwa chama hicho kuridhishwa na hatua ya awali ya Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ya Canada, Profesa John Thornton kuja kukutana na Rais Magufuli na kukubali kulipa fedha zote.

Polepole pia ametaka agizo la Rais Magufuli la kuchunguzwa kwa watu wote waliohusika, huku akitaka watu hao kutoa ushirikiano ili ujulikane ukweli ujulikane kwakuwa chama hicho kinataka kuona Watanzania wananufaika na rasilimali zao.

Amesema kitendo cha Rais Magufuli kuzuia maslahi ya watu wakubwa na mashirika makubwa kinahitaji moyo mkubwa wa kujitoa na wakizalendo kama alionao Rais Magufuli. Polepole pia alikiri kuwa yapo makosa yalifanyika kipindi cha nyuma lakini nkwa sasa chama hicho kinaanza upya kwa kuwa Watanzania wanataka kiwe kisafi.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment