Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo Machi 02,
2017 ameanza ziara ya kikazi ya siku 4 katika Mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.
Katika ziara hiyo Rais Magufuli atafungua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na
wananchi katika mikutano ya hadhara.
Leo asubuhi Rais Magufuli ataweka jiwe la msingi la kiwanda cha kutengeneza vigae (Tiles) cha Tanzania Goodwill Ceramic
Tiles Ltd. kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani na baadaye ataelekea Mkoani Lindi.
Kesho Machi 03, 2017 Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Lindi na
keshokutwa Machi 04, 2017 atafanya ziara yake Mkoani Mtwara.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment