Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 16 June 2017

SAMSUNG WAJA NA PROMOSHENI YA NUNUA SAJILI NA USHINDE

Meneja Mauzo Samsung, Lailatu Jethwa (kushoto) akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na kampeni yao mpya ya ‘Nunua sajili na Ushinde’ inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati  ni, Meneja wa Samsung Nchini,Rayton Kwembe na Meneja bidhaa za majumbani wa Samsung,Elias Mushi .
 Meneja Mauzo Samsung, Lailatu Jethwa (kushoto) akiwaonyesha  waandishi wa habari bidhaa zinazohusishwa katika kampeni yao mpya ya ‘Nunua sajili na Ushinde’ inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati  ni Meneja wa Samsung Nchini Rayton Kwembe,  akifatiwa na meneja bidhaa wa Samsung, Elias Mushi na Meneja wa Phyramid Consumers


Meneja Mauzo Samsung, Lailatu Jethwa (kushoto) akiwaonyesha  waandishi wa habari bidhaa zinazohusishwa katika kampeni yao mpya ya ‘Nunua sajili na Ushinde’ inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja wa Samsung Nchini Rayton Kwembe. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

*************

SAMSUNG Tanzania wameanzisha mfumo wa kuweka stika mbili katika bidhaa zao kwa ajili ya utambuzi wa bidhaa zao halisi pamoja na kupambana na bidhaa feki nchini. Sambamba na mkakati huo Samsung piawameanzisha Kampeni ya ‘Nunua Sajili na Ushinde’. 

Kampenihiyo ya mwezi mzima inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini itaanza tarehe 16 ya mwezi juni katika  mikoa yote ya Tanzania, na itaambatana na promosheni kabambe inayotarajiwa  kuwazawadia mamilioni ya watanzania  watakao nunua bidhaa halisi za Samsungkama vile TV, Friji, Microwave, mashine ya kufulia pamoja na Viyoyozi.

“Ukizingatia bidhaa feki zina hatarisha afya za watumiaji, mahitaji ya bidhaa bora na halisi yanaongezeka kwa kasi kila kukicha. Samsung tumeendelea kufanya jitihada zaidi katika kukidhi matakwa ya  wateja wetu ulimwenguni pamoja na Tanzania kwa ujumla. Samsung Tanzania inaamini kwamba kampeni ya ‘Nunua, Sajili, Na Ushinde’ itaongeza uzoefu mpya na uelewa  kwa wateja wetu wa dar es salaam na mikoani pia juu ya utambuzi wa bidhaa feki zisizo kuwa za Samsung” alisema Meneja Bidhaa kutoka Samsung,  Elias Mushi.

Akiongeleakuhusumkakati huo mpya Bw Mushi alisema ‘tumeongeza alama mpya kwenye bidhaa zetu ambazo ni stika mbili zitakazo wasaidia wateja kutambua bidhaa feki sokoni, Bidhaa za Samsung zitakuwa na stika mbili, stika msambazaji na stika inayotambulisha bidhaa halisi ya Samsung. Kampeni ya ‘Nunua Sajili na Ushinde’ itakua ni kiunganishi cha kupeleka elimu kwa wateja wetu ambayo itawapa taarifa za bidhaa zetu zinazoenda sambamba na mahitaji ya matumizi yao.

Pamoja na kampeni hiyo kabambe Samsung wataendesha bahati nasibu ambayo washindi watajinyakulia zawadi kila siku kwa muda wa mwezi mmoja. Wateja wa Samsung watafaidika na mpango huu kwa kusajili namba za bidhaa zao mara tu wanaponunua bidhaa hiyo. Hii itafanyika kwa kutuma namba ya bidhaa kwenda namba 0798222333. Wateja watapata meseji ya uthibitisho wa bidhaa halisi ya Samsung papo hapo. Kwa kufanya hivo Mteja atakuwa amejiunga moja kwa moja kwenye droo ambayo itamwezesha kuwa mshindi wa bidhaa bora za Samsung zinakuja na waranti ya miezi 12.

Kusherehekea uzinduzi huo wa Nunua Sajili na Ushinde pamoja na kusambaza elimu juu ya stika hizo mbili kwa watanzania Samsung inaendesha kampeni ya uhamasishaji nchi nzima kwa kipindi cha mwez mmoja.

Kwa kupitia mkutano wa vyombo vya habari uliofanyika makao makuu ya Samsung. Samsung wametangaza kuingia ubia wa usambazaji na kampuni ya Tanzania Pyramid Consurmers ltd. Makubaliano yamehusisha usambazaji wa bidhaa mpya na za kisasa za kieletroniki za Samsung. Makubaliano hayo yatapelekea makampuni hayo mawili kurahisisha upatikanaji wa bidhaa bora na halisi za Samsung ndani ya Tanzania.

Bidhaa za Samsung ambazo zinasambazwa mpaka sasa na Tanzania Pyramid Consumers ltd, ni pamoja na tv, friji, viyoyozi, mashine za kufulia pamoja na microwave.

Akifafanua kuhusu makubaliano hayo Bw Mushi alisema “tunafuraha kuungana na Tanzania pyramid consumers ltd kwenye usambazaj wa  bidhaa zetu. Tupo mbioni kutambulisha bidhaa zetu mpya na pia tumejipanga kuongeza uwepo wetu nchi nzima kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa bidhaa bora na halisi za Samsung nchini”  akaongeza kuwa “lengo letu ni kuendelea kuboresha huduma kwa wateja wetu kila Nyanja pamoja na kutanua wigo mpana wa mauzo pamoja na kuwafika wateja wetu maana wao ndo nguzo ya mafanikio yetu. Muungano wetu na Pyramid Consurmers umetufanya tuwafikie wateja wetu kwa urahisi, kwa haraka na kwa kuwapa mahitaji sahihi kwa kile wanachohitaji”

Karen Babu Meneja wa Pyramids consumers aliongezea kuwa “ Samsung ni kampuni kubwa inayozidi  kujitanua na yenye ubunifu wa hali ya juu kwenye  bidhaa zake hivyo tunajivunia kutumia uzoefu wetu na ujuzi tulionao kufanikisha malengo haya yote kwa pamoja. Pia tunajivunia kushirikiana na Samsung kwa pamoja tutafanikisha kufikia soko la Tanzania kwa kiwango cha juu”


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment