MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amezitaka kampuni zilizowekeza
katika sekta ya mafuta na gesi nchini kuhakikisha zinanunua huduma na
bidhaa zinazopatikana nchini. Anaandika Katuma Masamba.
Amesema hitaji la watoa huduma wa Kitanzania kunufaika linaendana na
sheria ya mafuta ya mwaka 2015 inayosisitiza katika ununuzi wa bidhaa na
huduma zinazopatikana ndani.
Samia ameyasema hayo wakati akizundua Jumuiya ya Watoa Huduma Katika
Sekta ya Mafuta na Gesi Tanzania (ATOGS) jijini Dar es Salaam ambapo pia
alipongeza uanzishwaji wa jumuiya hiyo kwa kuwa una lengo sawa na
Serikali ya Awamu ya Tano.
“Na pale ambapo huduma na bidhaa hazipatikani nchini, basi makampuni
hayo yanapaswa kununua kutoka kwenye makampuni ya ndani yenye wabia nje
ya nchi,” amesema Samia.
Alifafanua kuwa sheria hiyo imezingatia maslahi ya wananchi ikitaka
hisa za makampuni ya ndani kutopungua asilimia 25 na kwamba kwa kununua
bidhaa na huduma kutoka ndani ya nchi, Watanzania wengi walioko vijijini
watanufaika.
Nae Balozi Ombeni Sefue ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi wa ATOGS aliiomba Serikali kushirikiana na sekta binafsi katika kutekeleza Sera na Sheria.
"Watoa huduma hawa wamejiunga katika jumuia hii wakiwa na matarajio kwamba Serikali itashirikia kwa karibu na ATOGS katika kushughulikia changamoto na vikwazo vya kibiashara na pia kufungua fursa kwa wafanyabiashara waliopo Tanzania," alisema Balozi Sefue.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment