Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 20 March 2017

RC MBEYA AZINDUA PROGAMU MAALUM YA MALEZI YA 'INUKA ESTA' YA WAKINAMAMA WAKROSTO

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akizungumza kwenye uzinduzi wa Programu ya INUKA ESTA iliyoandaliwa na Kurugenzi ya Wanawake na Watoto ya KKKT Dayosisi ya Konde. 
Mkurugenzi wa Wanawake na Watoto KKKT Dayosisi ya Konde, Alice Mtui akisoma risala ya Uzinduzi wa Programu ya Inuka Esta mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla Askofu Mstaafu wa Kanisa la Anglican, John Mwela akitoa neno katika uzinduzi wa Programu ya INUKA ESTA iliyoandaliwa na Kurugenzi ya Wanawake KKKT Dayosisi ya Konde Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akipokea zawadi ya Keki kutoka kwa viongozi wa Kurugenzi wa Wanawake Baadhi ya Viongozi wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya baada ya kumaliza uzinduzi wa Programu ya INUKA ESTA
  Wanawake wa Kikristo wakiwa katika ukumbi wa Tughimbe wakifuatilia uzinduzi wa programu ya Inuka Esta
*******************
KURUGENZI ya Wanawake na Watoto ya Kanisa la Kiinjili Kilutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde imeshangazwa na uwepo wa utapiamlo na udumavu wa Watoto licha ya Mkoa wa Mbeya kuongoza katika uzalishaji wa mazao ya Chakula.

Kurugenzi hiyo ilibainisha kushangazwa huko katika Risala iliyosomwa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla wakati wa uzinduzi wa Programu za Wanawake ziitwazo INUKA ESTA.

Akisoma Risala hiyo, Mkurugenzi wa Wanawake na Watoto KKKT Dayosisi ya Konde, Alice Mtui alisema lengo la kuzindua Programu hiyo ambayo itabeba vipindi mbali mbali vya kuwaelimisha, kuwahamasisha na kuwainua Wanawake wa KKKT na kuwavuta wasio wakristo kuvaa uhusika wao,

Alisema lengo lingine ni kuhamasisha wanawake wa Jukwaa la kikristo Mbeya ili kuleta ukombozi kwenye maisha ya  familia na jamii na kurejesha hadhi na thamani ya utu pamoja na maadili yanayozidi kushuka na kuporomoka katika kizazi cha sasa.

Kuhusu uwepo wa Utapiamlo katika jamii, Mkurugenzi huyo alisema ni jambo la aibu kwa Mkoa wa Mbeya ambao ni kati ya mikoa mikubwa mitano inayolisha Nchi lakini ni Mkoa wenye Utapiamlo na udumavu wa akili kwa watoto.

“Sio kweli kwamba watu wa Mbeya hawawezi kulisha familia zao chakula kipo cha kutosha na WanaMbeya wanauwezo mkubwa wa kulisha familia zao lakini tatizo kubwa ni wazazi na walezi wengi hawako makini kufuatilia na kupangilia lishe katika familia zao” alisema Mtui.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla alisema Mkoa wa Mbeya unaongoza kwa kuwa na makanisa mengi lakini baadhi ya dini zinatoa doa kwa Mkoa kutokana na matendo maovu yanayotokea kila siku.

Alisema baadhi ya dini zinahamasisha waumini wao kufukua makaburi ili wawaombee marehemu na kuwafufua jambo ambalo haliwezekani, matendo ya kuzika watu wakiwa hai na wengine kuzuia watu kuzikwa baada ya kufariki.

Aidha alitoa wito kwa Wanawake kusaidia kukemea maovu katika jamii hususani uuzaji na unywaji wa pombe zilizopigwa marufuku kama viloba na kilimo cha Bhangi na matumizi ya dawa za kulevya.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment