Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Saturday 28 January 2017

VITUO VYA TRA VYA KUHAKIKI TIN KUFUNGULIWA JUMAMOSI NA JUMAPILI

TAARIFA KWA UMMA
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwajulisha wadau na umma kwa ujumla kwamba vituo vya kuhakiki Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) vitakuwa wazi siku ja jumamosi tarehe 28  Januari 2017 kuanzia saa 3:00 hadi 11:00 jioni na jumapili tarehe 29 Januari 2017 kuanzia saa 4:00 hadi saa 9:00 Alasiri.

Vituo hivyo kwa Ilala ni TRA Samora, 14 Rays - Gerezani na Shaurimoyo. Kinondoni ni Millennium Tower Kijitonyama, Kibo complex- Tegeta na Ofisi ya Kodi Kimara. Temeke ni Uwanja wa Taifa, Ofisi ya Kodi Kigamboni na Ofisi ya Kodi Mbagala.

Aidha Mamlaka inaukumbusha  umma kwamba tarehe ya mwisho wa kuhakiki TIN ni tarehe 31 Januari 2017. Hivyo ni vyema kwa wale wote ambao hawajahakiki TIN kufika katika vituo tajwa mapema ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza baada ya zoezi kufungwa rasmi 

"Pamoja Tunajenga Taifa Letu"

Imetolewa na Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi 
TRA - Makao Makuu


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment