Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 19 June 2017

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUTARISHA NA KUTOA VYETI VYA SHUKRANI KWA WADAU WA MAZINGIRA

Viongozi na Waumini ya Dini ya Kiislam mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye sala ya magharibi wakati Iftar maalum iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam.
 Raia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wakisoma Qasida kwenye Iftar maalum iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi cheti cha shukrani Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mutahaba kwa ushiriki na ufanikishaji wa maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa ilifanyika Butiama.
Wengine waliopokea vyeti hivyo ni TBC, Lake Gas, TBL, WWF na ZANTAS.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi cheti cha shukrani Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL,Roberto Jarrin  kwa ushiriki na ufanikishaji wa maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa ilifanyika Butiama. Wengine waliopokea vyeti hivyo ni TBC, Lake Gas, Clouds Media, WWF na ZANTAS.
Ndugu, Jamaa, Marafiki na Wadau kutoka sekta mbali mbali wakipata futari kwenye Iftar maalum iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam.
*********************
Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu,wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam, viongozi mbalimbali wa Serikali na wa vyama vya siasa katika halfa ya futari aliyoiandaa katika makazi yake Oysterbay Jijini Dar es Salaam.


Katika Hafla hiyo ya futari, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan alishiriki katika utoaji wa vyeti kwa wadau wa mazingira ambao walishiriki kikamilifu katika maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani iliyofanyika Kitaifa tarehe 4-June-2017 - Butiama mkoani Mara.


Baadhi ya taasisi zilizopatiwa vyeti na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ni Shirika la Utangazaji Tanzania- TBC, Clouds Media, Lake Gas limited, Tbl, Zantas Air na WWF.

Akizungumza kwa Niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika hafla hiyo ya futari, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe January Makamba alimshukuru Makamu wa Rais kwa kuanda futari hiyo katika mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwani amesema ni jambo zuri na linalompendeza Mwenyezi Mungu.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment