Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 19 June 2017

HABARI ZA HIVI PUNDE: BILIONEA RUGEMALILA NA SETH WAPANDISHWA MAHAKAMANI KISUTU LEO


Watuhumiwa  James Rugemalila (kulia) na Harbinder Sethiwakiwa chini ya ulinzi wa maafisa wa polisi na Magereza kabla ya kupandishwa kizimbani katika Mahakam ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
 Watuhumiwa  James Rugemalila (kushoto) na Harbinder Sethi wakiwa chini ya ulinzi wa maafisa wa polisi  walipofikishwa kizimbani katika Mahakam ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo. 
******************
WAFANYABIASHARA maarufu nchini, James Rugemalila na Harbinder Sethi wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka sita ikiwemo kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani milioni 22.1  na  Sh bilioni 309. Anaandika Fransisca Emmanuel wa Habarileo.

Watuhumiwa hao walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na kusomewa mashitaka hayo na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Paul Kadushi anayesaidiana na Wakili Mkuu wa Serikali, Faraja Nchimbi na Joseph Kiula wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU).

Mashitaka yao ni kula njama, kujihusisha na mtandao na uhalifu, (kughushi na kutoa fomu zilizoghushiwa (yanamkabili Seth) kujipatia fedha kwa udanganyifu na kusababisha serikali hasara.

Rugemalila na Seth wamekosa dhamana hivyo wanaenda mahabusu hadi kesi yao itakapotajwa tena kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, haina mamlaka ya kusikiliza mashitaka ya uhujumu uchumi hivyo maombi ya dhamana yanatakiwa kupelekwa Mahakama Kuu.

Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi. 


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment