Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 7 March 2017

RAIS MAGUFULI AWASILI DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 07 Machi, 2017 amewasili Mkoani Dodoma ambako pamoja na mambo mengine ataongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa, Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi.

Mhe. Dkt. Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM ataongoza kikao na mikutano hiyo kuanzia tarehe 10 - 12 Machi, 2017 Mjini Dodoma.

Mhe. Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewasili katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma akitokea Mkoani Morogoro ambako jana tarehe 06 Machi, 2017 alizindua uwanja wa kisasa wa ndegevita wa Ngerengere.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment