Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 5 March 2017

IGP MANGU AFANYA ZIARA YA KUDUMISHA UMOJA NA USHIRIKIANO NCHINI RWANDA

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Ernest Mangu (Kushoto), akiwasili nchini Rwanda, na kupokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini humo, (IGP) Emmanuel K. Gasana (Kulia) wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja jana, yenye lengo la kuimarisha mahusiano, kushirikiana na kufanyakazi kwa pamoja katika kudhibiti uhalifu na wahalifu hususan maeneo ya mipakani kwa lengo la kukuza uchumi baina ya nchi zote mbili ya Tanzania na Rwanda.


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Ernest Mangu, akiwa na mwenyeji wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Rwanda, (IGP) Emmanuel K. Gasana, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja nchini humo jana, yenye lengo la kuimarisha mahusiano, kushirikiana na kufanyakazi kwa pamoja katika kudhibiti uhalifu na wahalifu hususan maeneo ya mipakani kwa lengo la kukuza uchumi baina ya nchi zote mbili ya Tanzania na Rwanda

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Ernest Mangu (mbele kushoto) akitoa neno mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Rwanda, (IGP) Emmanuel K. Gasana, pamoja na ujumbe alioongozana nao nchini humo jana, katika ziara ya kikazi yenye lengo la kuimarisha mahusiano, kushirikiana na kufanyakazi kwa pamoja katika kudhibiti uhalifu na wahalifu hususan maeneo ya mipakani kwa lengo la kukuza uchumi baina ya nchi zote mbili ya Tanzania na Rwanda. BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI.



Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Ernest Mangu (kushoto), akimsikiliza mwenyeji wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Rwanda, (IGP) Emmanuel K. Gasana, akitoaneno mbele ya  wajumbe kutoka Tanzania (hawapo pichani) IGP Mangu, yupo nchini Rwanda, kwa ziara ya siku moja  yenye lengo la kuimarisha mahusiano, kushirikiana na kufanyakazi kwa pamoja katika kudhibiti uhalifu na wahalifu hususan maeneo ya mipakani kwa lengo la kukuza uchumi baina ya nchi zote mbili ya Tanzania na Rwanda.



Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Ernest Mangu (kushoto),  na mwenyeji wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Rwanda, (IGP) Emmanuel K. Gasana, wakibadilishana hati ya makubaliano yenye mkakati wa kuhakikisha nchi zote mbili ya Tanzania na Rwanda, zinakuwa salama hususan maeneo ya mipakani na hata kwenye barabara zote zinazotumiwa na wafanyabiashara, IGP Mangu, pamoja na ujumbe wake amefanya ziara ya kikazi nchini humo jana.


Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Ernest Mangu (kushoto), akipokea zawadi kutoka kwa mwenyeji wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Rwanda, (IGP) Emmanuel K. Gasana, mara baada ya kuitimisha ziara yake ya kikazi ya siku moja jana, yenye lengo la kuimarisha mahusiano, kushirikiana na kufanyakazi kwa pamoja katika kudhibiti uhalifu na wahalifu hususan maeneo ya mipakani kwa lengo la kukuza uchumi baina ya nchi zote mbili ya Tanzania na Rwanda.  (Picha zote na Demetrius Njimbwi- Jeshi la Polisi Tanzania)


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment